Rais Yoweri
Museveni wa Uganda, amesema kwa sasa amepona maambukizi ya virusi vya corona,
baada ya vipimo vya Covid-19 kuonyesha amepata maambukizi.
Kauli hiyo
ya Rais Museveni ameitoa jana, ikiwa ni baada ya kupita siku 11 za kujitenga
akipatiwa matibabu tangu kubaini kwamba anamaambukizi ya corona.
Rais
Museveni amesema awali alidharau dalili za maambukizi, lakini alipoanza kupatwa
na mafua ndipo alipomuita dokta ampime na kubaini amepata corona.
Haijajulina
mara moja ni kwa jinsi gani Rais Museveni ambaye amekuwa akifuata taratibu kali
za kujikinga na maambukizi ya Covid-19, amepata maambukizi hayo.
0 Maoni