Mwanamke mmoja nchini Ecuador amefariki dunia siku chache tu kupita, tangu waombolezaji kubaini kuwa bado yupo hai akiwa kwenye jeneza.
Mwanamke
huyo Bella Montoya, 76, alithibitishwa kuwa amefariki na daktari katika
hospitali moja iliyopo kwenye mji wa Babahoyo wiki iliyopita.
Wakati wakiomboleza,
waombolezaji walisikia jeneza linagongwa na walipofungua wakabaini bado yupo
hai na kumkimbiza hospitali.
Baada kulazwa
kwenye chumba cha wagonjwa mahututi siku saba, Wizara ya Afya Ecuador ilithibitisha
mwanamke huyo amefariki dunia siku ya Ijumaa.
0 Maoni