Putin aambiwa vita ya Ukraine lazima imalizike

Vita ya Ukraine lazima imalizike, Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amemuambia Rais wa Urusi Vladimir Putin.

Kauli ya Ramaphosa ameitoa alipokutana na Putin, St Petersburg siku ya Jumamosi akiwa ni sehemu ya ujumbe wa wamani wa nchi sita za Afrika.

Ijumaa, Rais Volodymyr Zelensky, aliuambia ujumbe huo ataingia katika mazungumzo ya amani pale tu Urusi itapoondoka katika ardhi ya Ukraine.

Katika maongezi yao na Putin aliwaambia viongozi hao wa Afrika kwamba Ukraine imekuwa ikikataa kufanya mazungumzo ya amani.

Katika mkutano wa St Petersburg, Ramaphosa alitoa wito kwa pande zote kurejesheana wafungwa wa kivita na Urusi kuwarudisha watoto wanaodaiwa kuwachukua.

Chapisha Maoni

0 Maoni