Nyambizi
yenye watalii waliokuwa wanaenda kuangalia mabaki ya meli iliyozama ya Titanic
katika pwani ya kaskazini ya Amerika imetoweka kwenye bahari ya Atlantic.
Vikozi vya ulinzi
vya pwani ya Marekani vinakadiria kuwa nyambizi hiyo imebakiwa na saa 70 au 90,
kabla ya mitungi ya dharura ya hewa ya oksijeni haijaisha.
Chombo hicho
kina nahodha mmoja, na wataalam wanne wa msafara huo, kilianza kupigambizi siku
ya Jumapili asubuhi.
Nyambizi ilipoteza
mawasiliana baada ya muda wa saa moja na dakika 45, ilipopiga mbizi kwenda
kuona mabaki ya Titanic, kwa mujibu ya Walinzi wa Pwani wa Marekani.
Mmoja ya
watu wanaoaminika kwamba walikuwamo kwenye nyambuzi hiyo ni mfanyabiashara
Muingereza na mvumbuzi Hamish Harding.
Mabaki ya
meli ya Titanic yapo umbali wa mita 3,800m kwenye kina cha maji ya bahari,
katika sakafu ya bahari.
0 Maoni