Mwanamke Mjerumani aliyejiunga na kundi la Dola ya Kiislam (IS), amefungwa miaka tisa jela kwa uhalifu ukiwamo wa kuwafanya watumwa wanawake wa kabila la Yazidi.
Mwanamke
huyo mwenye umri wa miaka 37, pia alitiwa hatiani kwa uhalifu dhidi ya binadamu
na kuwa mwanachama wa kundi la kigeni la kigaidi.
Mahakama ya mji
wa magharibi wa Koblez, imesema mwanamke huyo aliwatesa wanawake wa Yazidi kwa
miaka mitatu akiwa anaishi huko Syria na Iraq.
Pia Mahakama
imebainisha kwamba mwanamke huyo alikuwa anamhamasisha mume wake kuwabaka na
kuwapiga wanawake hao wa kabila la Yazidi.
0 Maoni