Timu ya
Arsenal imekubali kulipa dau inalohitaji Chelsea la paundi milioni 65 ili kumuuza
mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani Kai Havertz.
Imefahamika
kuwa klabu hizo zimefikia makubaliano ya msingi, yanayotoa nafasi kwa mchezaji
huyo kujadili maslahi yake na kufanyiwa vipimo vya afya.
Ada ya Havertz,
ambaye amefunga magoli tisa katika michezo 47, akiwa na Chelsea msimu uliopita,
itakuwa na nyongeza akipata mafanikio.
Havertz, 24,
alijiunga na Chelsea akitokea timu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani mwaka 2020 kwa
dau la paundi milioni 71.
0 Maoni