Akichangia hotuba
ya bajeti ya 2023/2024 Mbunge wa Viti Maalum Mh. Salome Makamba amesema kwamba,
vifaa vinavyotumika kwa ujenzi wa makazi vinajulikana viwekwe alama ili viuzwe
kwa bei nafuu kwa wananchi.
“Serikali
mwaka jana iliongeza kodi kwenye nondo na mabati, mwaka huu kwenye sementi,
hivi mnataka tukaishi kwenye nyumba za udongo?” alihoji Mh. Salome.
Amesema anaelewa
lengo la Serikali kwa kuwa sekta inayozalisha sementi, nondo/chuma na mabati
inabiashara kubwa sana, lakini wasisahauliwe Watanzania wa kawaida ambao
wanatumia bidhaa hizo kujiboreshea maisha.
“Serikali
inamifumo yake ambayo inaweza kujua manunuzi haya yanafanyika kwa ajili ya
viwanda, miundombinu na manunuzi haya yanafanyika kwa ajili ya wananchi
kujiboreshea mazingira yao ya kuishi,” alisema Mh. Salome.
0 Maoni