Ombi la pili
la Manchester United la dau la paundi milioni 50 ili kumnasa kiungo wa Chelsea
Mason Mount, limekataliwa.
Mount, 24, anawaniwa
na Meneja wa United Erik ten Hag, katika kuimarisha kikosi chake baada ya kufuzu
kutinga Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.
Chelsea iliyotumia
paundi milioni 600 msimu uliopita, inapaswa kuwauza wachezaji wake kabla ya
Juni 30, ili kukidhi matakwa ya Financial Fair Play.
Timu ya Chelsea
inajua kuwa thamani ya Mount inafikia kiasi cha paundi milioni 70.
0 Maoni