Mtoto wa Rais
wa Marekani Joe Biden, Hunter Biden anatarajiwa kukiri makosa mawili, katika
kujaribu kuepuka kifungo cha jela.
Hunter
anakabiliwa na makosa ya kukwepa kodi, pamoja na kukiri kumiliki silaha akiwa
anatumia madawa ya kulevya, baada ya uchunguzi wa miaka 5.
Mwanasheria amewasilisha
nyaraka zinazoashiria makubaliano ya kukiri makosa na anatarajiwa kukubali
matibabu ya kuachana na dawa za kulevya.
Kwa
nadharia, bado anakabiliwa na kifungo cha mwaka mmoja jela katika kila kosa la
kodi na miaka 10 jela kwa kosa la silaha.
Makubaliano
ya kuepuka kifungo yanahitaji kuthibitishwa na jaji anayesikiliza kesi hiyo,
ambaye pia ataamua aina ya adhabu.
0 Maoni