Timu ya
Arsenal imekubali kumsajili mchezaji kiungo wa West Ham, Declan Rice, kwa dau
la paundi milioni 105.
Mazungumzo
yanaendelea baina ya klabu hizo mbili, kuhusu namna makubaliano yao hayo
yatakavyotekelezwa.
Hii ni baada
ya Arsenal kutoa ofa ya tatu, baada ya ofa zao mbili za mwanzo kukataliwa kwa
kutoa dau la chini ya paundi milioni 100.
Awali, Manchester
City, ambao walitoa ofa ya paundi milioni 90 iliyokataliwa Jumanne, walijiondoa
kwenye mbio za kunasa saini ya Rice.
0 Maoni