Aliyekufa ajali ya nyambizi Titan alipanga kupanda Kilimanjaro

 

Mmoja wa wanaume watano waliothibitishwa kufa kwenye nyambizi ya Titan Dubai, Hamish Harding (58), alipanga kuja kupanda Mlima Kilimanjaro akiwa na wanafamilia yake na washkaji zake wanaofikia 20 Julai, 2023, baada ya matamanio yake hayo awali kukwama kutokana na Uviko-19.

Waliokufa ni Hamish Harding, 58, Shahzada Dawood, 48, na mwanae Suleman Dawood, 19, Paul-Henri Nargeolet, 77, pamoja na Stockton Rush, 61.

Harding ana rekodi tatu za dunia za Guinness, wakati mwaka 2021 aliweka rekodi ya kuwa mmoja wa wanadamu waliofanikiwa kwenda sehemu ya chini kabisa duniani alipotembelea handaki la baharini la #marianatrench akitumia saa 36 majini na chombo kilichoitwa #challengerdeep.

Mwaka huu Harding alipanga kufanya #royaltourtanzania, akidhamiria kufika kwenye kilele cha juu zaidi duniani kilichosimama chenyewe kwa kufika@#mountkilimanjaro.

Chapisha Maoni

0 Maoni