Mwanamuziki Tina Turner, ambaye vibao vyake vikali vya The Best na What's Love Got to Do With It vilimpatia umaarufu mkubwa, amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 83.
Turner alikuwa anakabiliwa na matatizo kadhaa ya kiafya
katika miaka ya hivi karibuni yakiwemo ya saratani, kiharusi na figo kushindwa
kufanyakazi.
Mwanamuziki huyo alipata umaarufu pamoja na mumewe Ike
katika miaka ya 1960 kwa nyimbo zao zikiwemo za Proud Mary na River Deep, Mountain
High.
Mnamo mwaka 1978 alitengana na Ike ambaye alikuwa
akimfanyia vitendo vya ukatili, na kuendelea kuimba peke yake na kupata
mafanikio zaidi katika miaka ya 1980.
Turner aliyepachikwa jina la Malkia wa Rock 'n' Roll, alikuwa
maarufu kwa uchezaji wake wa mitego na kutumia nguvu jukwaani pamoja na sauti
yake kali.
0 Maoni