Mvurugano Jubilee Uhuru akimbilia kwa msajili

 


Pande mbili zinazokizana katika kilichokuwa chama tawala Kenya cha Jubilee, zimekimbilia kwa Msajili wa Vyama vya Siasa Anne Nderitu ili amalize mgogoro wao wa kuwania madaraka, ambapo kila upande unataka kuwatimua kwenye chama wenzao.

Upande unaoongozwa na rais mstaafu Uhuru Kenyatta, umeiandikia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakitaka mbunge wa kuchaguliwa Sabina Chege aliyeanzisha uasi na kuteuliwa kuwa kiongozi wa chama pamoja na mbunge Kanini Kega kufutwa uanachama.

Kenyatta anawatuhumu wabunge hao wawili kwa kukiuka Katiba ya chama kwa kuunga mkono sera za Rais William Ruto za chama cha UDA.

Kama hiyo haitoshi, wabunge hao wawili pia wamekuwa wakituhumiwa kwa kuanzisha uasi dhidi ya viongozi wa chama cha Jubilee, jambo ambalo ni ukiukaji mkubwa wa  Katiba ya chama.

Chapisha Maoni

0 Maoni