SIMANZI
Watoto wawili wa familia moja wamefariki dunia na mmoja kunusurika kifo baada ya kudaiwa kulishwa sumu na baba yao mzazi.
Tukio hilo limetokea katika eneo la Kwangwale Chanika Ilala Jijinj Dar es Salaam kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni mgogoro wa kifamilia baina Karim Chamwande na mke wake.
MWENYEKITI AFUNGUKA
Mwenyekiti wa mtaa huo Bakari Seif amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo limetokea tarehe 23 mwezi April majira ya saa 10 usiku wa kuamkia Idd Pili baada ya majirani kushtuka kuwepo na tukio hilo.
Ibrahimu anaeleza kuwa watoto hao watatu walikuwa wakiishi na mama wa mzazi wa mtuhumiwa Karimu ambaye yeye alikuwa akiishi peke yake baada ya kutengana na mkewe katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
Chanzo:TBC1
0 Maoni