Kauli hii ya Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa, kwamba:"𝐔𝐤𝐢𝐨𝐧𝐚 𝐦𝐭𝐮 𝐚𝐧𝐚𝐭𝐚𝐤𝐚 𝐤𝐮𝐡𝐚𝐫𝐢𝐛𝐮 𝐚𝐦𝐚𝐧𝐢 𝐮𝐣𝐮𝐞 𝐚𝐧𝐚𝐮𝐡𝐮𝐣𝐮��𝐮 𝐮𝐡𝐮𝐫𝐮 𝐰𝐞𝐭𝐮. 𝐓𝐮𝐬𝐢𝐤𝐮𝐛𝐚𝐥𝐢 𝐤𝐮𝐭𝐮𝐦𝐢𝐰𝐚 𝐤𝐮𝐯𝐮𝐫𝐮𝐠𝐚 𝐭𝐮𝐥𝐢𝐜𝐡𝐨 𝐤𝐢𝐣𝐞𝐧𝐠𝐚 𝐤𝐰𝐚 𝐦𝐢𝐚𝐤𝐚 𝐦𝐢𝐧𝐠𝐢." inaendelea kuwa dira na msingi wa kitaifa. Kauli yake inawakumbusha Watanzania kuwa kuharibu amani ni sawa na kuhujumu uhuru wao wenyewe, na hivyo wajibu wao ni kulinda tunu hii iliyojengwa kwa misingi imara kwa miaka mingi.
Tanzania
imeendelea kutambulika kama moja ya nchi salama zaidi barani Afrika, sifa
ambayo imekuwa chachu ya ukuaji wa sekta muhimu za kiuchumi kama vile utalii,
kilimo, na viwanda.
Hali hii
inathibitisha kuwa amani na mshikamano imara ni msingi wa ustawi wa wananchi na
maendeleo endelevu ya taifa. Huku shughuli za maisha zikiendelea kama kawaida
nchini kote, wito wenye nguvu umetolewa kwa Watanzania wote kulinda kwa wivu
mkubwa tunu hii ya amani, utulivu, na umoja.
Katika kudumisha
mafanikio haya, kuna mambo makuu yaliyosisitizwa ambayo kila Mtanzania anapaswa
kuyazingatia. Kwanza, ni muhimu kuendelea kudumisha muungano, uhuru, umoja, na
mshikamano baina ya Watanzania wote. Hili linahakikisha taifa linaendelea
kupiganiwa kwa wivu mkubwa na kuendelea kuwa kimbilio la amani.
Pili, wananchi
wanahimizwa kupuuza maneno ya wahuni na vibaka wachache walio nje ya nchi ambao
wanalipwa na kufanya kazi kwa malengo ya kugawanya Watanzania, kuchochea
vurugu, na kuvunja amani ya taifa.
Aidha, kila
mwananchi anatakiwa kuendelea kuamini kuwa Tanzania ni moja, na hakuna nchi
nyingine. Inasisitizwa kuwa endapo tutavuruga amani ya taifa letu, basi hatuna
pakwenda, kwani Tanzania ni moja tu duniani kote, hivyo ni wajibu wetu
kuendelea kulilinda taifa letu. Kwa upande wa imani, ni muhimu kwa Watanzania
wote kuendelea kuwa wamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kutusaidia na
kudumisha amani ya taifa letu, kwani bila amani hakuna maendeleo
yatakayopatikana.
Ujumbe mkuu unabaki: "𝐀𝐤𝐢𝐥𝐢 𝐲𝐚 𝐤𝐮𝐚𝐦𝐛𝐢𝐰𝐚 𝐜𝐡𝐚𝐧𝐠𝐚𝐧𝐲𝐚 𝐧𝐚 𝐲𝐚 𝐤𝐰𝐚𝐤𝐨, 𝐰𝐚𝐩𝐮𝐮𝐳𝐢 𝐰𝐨𝐭𝐞 𝐰𝐚𝐧𝐚𝐨𝐭𝐚𝐤𝐚 𝐤𝐮𝐭𝐮𝐠𝐚𝐰𝐚 𝐭𝐮𝐰𝐚𝐩𝐮𝐮𝐳𝐞, 𝐭𝐮𝐮𝐧𝐠𝐚𝐧𝐞 𝐤𝐮𝐝𝐮𝐦𝐢𝐬𝐡𝐚 𝐦𝐮𝐮𝐧𝐠𝐚𝐧𝐨 𝐰𝐚 𝐭𝐚𝐢𝐟𝐚 𝐥𝐞𝐭𝐮."

0 Maoni