Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Tanzania

 

Mbunge wa Jimbo la Ilala kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Mussa Azzan Zungu, amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata kura 378 kati ya kura 380 zilizopigwa na wabunge.

Uchaguzi huo umefanyika leo, Novemba 11, 2025, katika Ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma, ambapo Zungu amewashinda wagombea wengine watano waliokuwa wakigombea nafasi hiyo kupitia vyama vya NRA, DP, ADC, NLD, na AAFP.

Zungu, ambaye alikuwa Naibu Spika wa Bunge katika Bunge lililopita, sasa anakuwa rasmi kiongozi wa mhimili huo wa dola, katika Bunge la 13 lililoanza rasmi leo jijini Dodoma.

Aliyekuwa Spika wa Bunge lililomalizika, Dkt. Tulia Ackson, alijitoa katika mbio za kuwania tena nafasi hiyo siku chache zilizopita bila kueleza sababu za uamuzi wake huo.

Chapisha Maoni

0 Maoni