Uzalendo ni kujenga: Tuthamini na kulinda mali ya taifa letu

 

Vitendo vya kuharibu miundombinu kama vile kuchoma magari ya umma (BRT) vimekosolewa vikali, vikitajwa kama kukosa Uzalendo na kujiharibia wenyewe. Uzalendo wa kweli una maana ya kuthamini na kulinda rasilimali na miundombinu ya taifa, kwa kuwa ndiyo inayosaidia maisha ya mamilioni.

Siraji Ali anahoji kwa uchungu: "Serikali iliona kuna umuhimu wa kuleta magari mapya, leo hii yamechomwa moto sasa hii inakuathiri mwenyewe; ulidai upewe kitu umepewa leo hii unakuja kukiunguza. Sasa faida ni ya nani?" Anaongeza kuwa hata wafanyabiashara wakubwa wameathirika kwa sababu "mzunguko wa kawaida wa maisha haukuwepo."

Faizat Peter alikumbusha kuwa "huo sio utanzania," na kwamba lazima tujifunze yasitokee tena.

Aidha Siraji katika mahojiano alisema kwamba madhara hayakuwa kwa Tanzania pekee bali hata nchi jirani ambazo zinategemea utulivu wa Tanzania kupitisha mahitaji yao.

"Tanzania ni lango kuu la nchi jirani. Vurugu hizi zimeathiri hata nchi jirani ambazo zinategemea Bandari yetu. Uzalendo ni pia kutambua jukumu letu katika ukanda, na kuilinda amani yetu ni kulinda uchumi wa nchi zingine."

Alisisitiza kuwa vitendo vya uharibifu vilivyofanywa ni uhaini wa kiuchumi dhidi ya Watanzania na jirani zao.

Chapisha Maoni

0 Maoni