Polisi wamkamata mwanajeshi wa Marekani akiwa na mabomu

 

Jeshi la Polisi mkoani Tarime/Rorya limemkamata mwanaume mwenye uraia pacha wa Marekani na Kenya, Charles Onkuri Ongeta (30), ambaye pia ni mwanajeshi wa Jeshi la Marekani mwenye cheo cha Sajenti, akiwa na mabomu manne ya kurushwa kwa mkono aina ya CS M68.

Tukio hilo lilitokea Novemba 16, 2025 imesema Ongeta alikamatwa mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Sirari, wakati askari wa ulinzi wa mipaka walipomsimamisha mtuhumiwa huyo aliyekuwa akiingia nchini akitokea upande wa Kenya kwa kutumia gari lenye namba KDP 502 Y, aina ya Toyota Land Cruiser.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi, silaha alizokutwa nazo haziruhusiwi kuingizwa nchini hata kama angekuwa ameomba kibali, kwani sheria za umiliki wa silaha nchini hazitumii vibali kwa vifaa vya aina hiyo.

Jeshi la polisi limesema linaendelea kukusanywa ushahidi sambamba na kuhojiwa kwa tuhuma hizo ili hatua stahiki kwa mujibu wa sheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake.

Jeshi la Polisi limesema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini lengo la mtuhumiwa kuingia nchini akiwa na mabomu hayo, huku akiendelea kushikiliwa kwa mahojiano zaidi.



Chapisha Maoni

0 Maoni