Mhe. Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Tanzania

 

Mbunge wa jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu, ameshinda nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano la 13 kwa kupata kura 348, huku mgombea mwenzake Steven Masele akiambulia 16 pekee.

Katika uchaguzi huo nafasi ya Unaibu Spika ilitwaliwa na Mhe. Daniel Sillo aliyeibuka kidedea baada ya kupata kura 362, huku wagombea wengine waliokuwa wamejitokeza awali wakijitoa kabla ya upigaji kura kuanza.

Kwa uchaguzi huo uliofanyika leo Jijini Dodoma sasa ni rasmi Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepata viongozi wapya wa muhimili huo wa Serikali baada ya kufanyika kwa uchaguzi wa Spika na Naibu Spika jijini Dodoma.

Katika Bunge lililopita, Mhe. Mussa Azzan Zungu alikuwa Naibu Spika wa Bunge, huku Dkt. Tulia Ackson ambaye alijitoa mapema kwenye mbio za kuwania Uspika alikuwa ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano.

Taarifa kutoka Bungeni zinaeleza kuwa jumla ya kura mbili (2) ziliharibika wakati wa mchakato huo wa uchaguzi, ambao ulifanyika kwa uwazi na kufuata kanuni za Bunge

Chapisha Maoni

0 Maoni