TMDA yatoa mafunzo ya dawa bandia na zisizosajiliwa kwa wafamasia Mloganzila

 

Idara ya famasia kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila imepatiwa mafunzo kutoka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kuhusu dawa zisizo na ubora, dawa bandia na dawa zisizosajiliwa ili kuendelea kutoa huduma bora za dawa kwa wagonjwa.

Akitoa mafunzo hayo mtoa mada kutoka TMDA mfamasia na mkaguzi Keddy Manga amesema wafamasia wanatakiwa kuzingatia ubora, usalama na ufanisi wa dawa wanazopokea na kuzitoa kwa wagonjwa.

Mafunzo hayo yametolewa kwa  lengo la kuwasaidia wafamasia wa hospitali kubaini dawa ambazo hazijasajiliwa nchini(unregistered), dawa na vifaa tiba visivyo na ubora (substandard) , dawa na vifaa tiba bandia (counterfeits) pamoja na kuangalia rangi ya dawa na maandishi ya lebo.



Chapisha Maoni

0 Maoni