Mgombea Urais wa CCM azuru kaburi la Baba wa Taifa

 

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiomba dua kwenye Kaburi la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Kijiji cha Mwitongo, Butiama mkoani Mara tarehe 10 Oktoba, 2025.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasha mshumaa katika Kaburi la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Kijiji cha Mwitongo, Butiama mkoani Mara tarehe 10 Oktoba, 2025.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiweka shada la maua katika Kaburi la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Kijiji cha Mwitongo, Butiama mkoani Mara tarehe 10 Oktoba, 2025.

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 10 Oktoba, 2025 ametembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika eneo la Mwitongo, Wilaya ya Butiama.

Akiwa katika eneo hilo, Mhe. Dkt. Rais Samia amezuru kaburi la Mwalimu Nyerere na amezungumza na wanafamilia wakiongozwa na Mlezi wa familia ya Mwalimu Nyerere Chifu Japhet Wanzagi.

Mhe. Rais ambaye pia ni mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi yupo katika Mkoa wa Mara kuanzia jana tarehe 09 Oktoba, 2025 akiendelea na kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Baada ya hapo Mhe. Dkt. Samia ameendelea na kampeni zake leo katika Wilaya za Butiama na Serengeti katika Mkoa wa Mara na Bariadi katika Mkoa wa Simiyu.

Chapisha Maoni

0 Maoni