Mgombea Mwenza
wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi,
ameendelea na mikutano yake ya kampeni za lala salama kwa kishindo leo Oktoba
22, 2025, katika uwanja wa mpira wa John Mwakangale, Kyela mjini, mkoani Mbeya.
Mkutano
huo wa hadhara umehudhuriwa na maelfu ya wakazi wa Kyela, waliokusanyika
kumsikiliza Dkt. Nchimbi ambaye alitumia jukwaa hilo kueleza mafanikio ya
serikali ya awamu ya sita na kuomba ridhaa ya wananchi kwa mara nyingine kuichagua
CCM.
Dkt.
Nchimbi alisisitiza kuwa serikali inayoongozwa na mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeleta mageuzi makubwa katika
sekta mbalimbali kama vile afya, elimu, miundombinu na uchumi wa viwanda.
Alieleza
kuwa ushindi wa CCM katika uchaguzi mkuu ujao utaendeleza mafanikio haya na
kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa nchi ya mfano barani Afrika kwa maendeleo
na amani.
Katika
hotuba yake, alitoa wito kwa wananchi wa Kyela na Watanzania kwa ujumla
kujitokeza kwa wingi kupiga kura Oktoba 29, 2025, ili kuhakikisha ushindi wa
kishindo kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wagombea ubunge na udiwani wa
CCM. Alieleza kuwa kura ya kila mmoja ni muhimu na ni silaha ya kuleta
maendeleo endelevu kwa taifa.
Mkutano huo
ulihudhuriwa pia na viongozi wa chama, wagombea ubunge na udiwani wa CCM katika
jimbo hilo, ambapo walitumia nafasi hiyo kuwasilisha ahadi na mipango yao kwa
wananchi. Kampeni hizi ni sehemu ya harakati za lala salama ambazo zinatarajiwa
kukamilika kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu unaosubiriwa kwa hamu kote
nchini.



0 Maoni