Maadhimisho ya Kumbukizi ya Mwl. Nyerere, Hifadhi ya Wanyamapori ya Pande

 

Katika kuadhimisha kumbukizi ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania- TAWA jana Oktoba  14, 2025, imepokea zaidi ya watalii 100 kutoka Jumuiya ya Mtakatifu Columba kutoka Parokia ya Bikira Maria Imakulata -Msakuzi waliokuja kujionea uzuri wa pekee wa Hifadhi ya Wanyamapori ya Pande, jijini Dar es Salaam.

Hifadhi ya Pande ni hazina iliyojificha, lakini leo, imefunua uzuri wake halisi. Watalii walipata nafasi ya kipekee kujionea wanyamapori mbalimbali kama vile Simba, Duma, Mamba, na Chatu, Pundamilia, Swala, Mbuni na Nyumbu.

Mandhari tulivu ya misitu, sauti za ndege wa porini, na wanyama waliopo kwa wingi ziliwafanya wageni wafurahie kila dakika ya ziara yao.

“Hatukutegemea kuona wanyama wengi kiasi hiki tukiwa bado Dar es Salaam”, alisema Evodius Gasper, miongoni mwa watalii kutoka Jumuiya ya Mt. Columba.

Watalii hawa waliahidi kuwa mabalozi wa Hifadhi ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Pande.




Chapisha Maoni

0 Maoni