Mgombea
urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Dkt. Samia
Suluhu Hassan amewaambia vijana nchini kwamba Tanzania yao ni mahali pazuri na
kuwasihi wasidanganyike kuiharibu nchi yao.
Dkt.
Samia amewaambia vijana kwamba Tanzania ni pepo ukilinganisha na nchi nyingine
za Kusini mwa Afrika na Afrika ya Kati.
Mgombea
huyo wa urais kupitia CCM ameyasema hayo jana Oktoba 23, 2025 alipohutubia
mkutano mkubwa wa kuhitimisha kampeni zake Mkoani Dar es Salaam uliofanyika
katika Viwanja vya Tanesco Vituka wilayani Temeke.
Mkutano
huo ulioshirikisha majimbo ya Temeke, Mbagala, Chamazi na Kigamboni, ulikuwa wa
mwisho kwa kampeni zake Tanzania Bara, akiwa amefanya ziara za kampeni katika
mikoa yote 26 ya Bara. Amabpo leo Oktoba 24, 2025 Dk Samia atahitimisha kampeni zake
Tanzania.
Zanzibar
kwa kuhutubia wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi kwenye Viwanja vya
Kibandamaiti.
"Kwenye
nchi yenye jina, yenye sifa zake yenye kuendeleza watu wake, msidanganywe wale
waliopo nje huko wasiwadanganye, hapa ni pazuri kwelikweli mkipata fursa tu ya
kuingia kwa majirani zetu
hapo,
kaangalie vijana wenzenu wanavyokula ndumu unaweza ukasema mimi narudi
Tanzania," Dkt. Samia aliwaambia maelfu ya wananchi wakiwamo vijana wa majimbo
hayo.
Ameongeza:
"Tanzania ndio kwetu, kwa hiyo niwaambie vijana sisi wazazi wenu tunapita,
nchi hii inawategemea ninyi, tunatarajia ninyi (vijana) tuwaachie nchi hii
muiendeshe kama tunavyoiendesha.
Kwahiyo
vijana wa Tanzania msidanganywe hata kidogo na katika kuendesha nchi
tumetengeneza mifumo mizuri sana ambayo kila baada ya miaka mitano tunachaguana
namna ya kuongoza nani ashike nafasi gani, katika ngazi tofauti, hakuna maeneo
mengine wanangu".
Amewataka
vijana kutuliza munkari kwani nchi ni mali yao na hakuna mwenye cheti cha
kusema ni yake.
"Wengine
wanasema sisi tunawakilisha wananchi, wananchi ni kina nani, wananchi ni ninyi
hapa na wengine na wengine na wengine, hakuna mwenye milki ya wananchi. Hapa
tunapeana majukumu tu we shika jukumu hili, wewe hili, kwa hiyo nawaomba vijana
wangu msiharibu nchi yenu, msiharibu amani ya nchi yenu fuateni serikali yenu
inavyowaelekeza, fuateni, Katiba yenu inavyowaelekeza, fuateni sheria za nchi
zinavyowaambia, zinavyotaka, mtaishi kwa salama, mtaishi kwa amani
hamtasumbuliwa," amesema Dkt. Samia.
Amesisitiza
wote waliojiandikisha kupiga kura, wakapige kura Oktoba 29, mwaka huu bila
hofu.
"Mama yuko macho anawalinda, vyombo vyetu
vya ulinzi na usalama vipo macho vinawalinda. Kama yamewashinda wao sisi tupo tunaendelea
na ujenzi wa nchi yetu," amesema Dkt. Samia aliyetumia dakika 30 kuhutubia
mkutano huo.
Aidha,
amesema mkutano huo umehudhuriwa na vyama rafiki ambavyo amesema vimekuja
nchini kusoma ili wakati wa uchaguzi na wao wakafanye vipi Kwa vile CCM ni chama
kikubwa na ndio maana wapo hapa.
Alivitaja
vyama rafiki vilivyowaunga mkono ni SWAPO cha Namibia, Chama Cha Kikoministi
cha China, ANC cha Afrika Kusini, na NRM cha Uganda.
Akigusia
falsafa za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alisema ili tupate maendeleo
tunahitaji mambo manne - watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora.
Alifafanua kuwa CCM katika miaka mitano ijayo
itajikita zaidi katika masuala hayo ikiwemo watu kwa ajili ya kusimamia utu wa
mtu, utu wa Mtanzania katika kupata chakula, huduma za afya, maji safi na
salama,
umeme na
makazi ambavyo yote yamefanyiwa kazi.Alisema kisichoguswa ni makazi lakini watu
binafsi wanajenga, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linajenga nyumba nchi nzima
ili kuwapatia makazi bora watu.
Alisema
katika uchumi wamefanya vizuri katika uchumi mkubwa na uchumi mdogo.
Naye
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Asha- Rose Migiro amesema Dkt. Samia amekuwa bingwa wa
sekta ya sanaa, ubunifu na michezo nchini, ambako amekuwa akinunua bao kwa
michuano ya kimataifa maarufu Goli la Mama.
Naye
Mwenyekiti wa UWT Taifa na Mratibu wa kampeni Kanda ya Dar es Salaam, Mary
Chatanda alisema ametumwa na wanawake wa Tanzania karibu milioni 15.7, kuwa
wapo tayari kumpa kura za kishindo Dkt. Samia kutokana na kuliheshimisha taifa
kwa miaka minne aliyokaa madarakani kwa kuleta maendeleo makubwa katika nyanja
zote za kiuchumi na kijamii.
Kwa
upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi
Mahamoud Thabiti Kombo amesema Dkt. Samia anafanya kazi Kwa vitendo sio maneno,
katika kuleta maendeleo na ajira kwa vijana ndani na nje ya nchi.
Amesema
leo wamepata mkataba wa ajira 50,000 za Watanzania hususani vijana kwenda
kufanya kazi nje ya nchi huku nyingine 20,000 zipo njiani zinakuja.
Na, Aboubakary
Liongo -Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Idara ya Itikadi, Uenezi na
Mafunzo CCM

0 Maoni