TFS, STEP waanza utekelezaji wa mkakati wa kulinda Ikolojia ya Udzungwa - Kilombero

 

Kamishina wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo,  ameongoza kikao na timu ya STEP-Programme ikiongozwa na Mkurugenzi wa Mkakati wa Usimamizi wa Ikolojia ya Udzungwa, Dk. Trevor Jones, akiambatana na Meneja wa Ikolojia Frank Linhwa.

Katika kikao hicho kilichofanyika jana, pande zote zimekubaliana kuanza utekelezaji wa mpango mkubwa wa uwezeshaji katika ulinzi shirikishi wa misitu, ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa vitendea kazi kama magari, mafunzo kwa watumishi na mikakati endelevu ya kuhifadhi bioanuai katika eneo la Ndwele. Hatua hii inalenga kuimarisha jitihada za TFS katika kulinda na kutunza ikolojia inayounganisha Misitu ya Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Udzungwa na Kilombero.

Aidha, imeelezwa kuwa matukio kadhaa ya kuimarisha ushirikiano kati ya TFS na STEP yamepangwa kutekelezwa katika siku zijazo, ili kuhakikisha ikolojia hii muhimu inabaki salama kwa manufaa ya taifa na vizazi vijavyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni