Mke wa Rais wa Ufaransa kuwasilisha ushahidi Marekani kuwa ni mwanamke

 

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na mkewe, Brigitte, wanapanga kuwasilisha ushahidi wa picha na wa kisayansi katika mahakama ya Marekani ili kuthibitisha kwamba Bi. Macron ni mwanamke.

Wakili wao amesema kuwa rais wa Ufaransa na Bi. Macron watawasilisha nyaraka hizo katika kesi ya kashfa waliyoifungua dhidi ya mshawishi wa mrengo wa kulia, Candace Owens, baada ya Owens kueneza imani yake kwamba Brigitte Macron alizaliwa mwanaume.

Mawakili wa Bi. Owens wamejibu kwa kuwasilisha ombi la kufuta madai hayo.

Akizungumza na podikasti ya BBC Fame Under Fire, wakili wa familia ya Macron, Tom Clare, alisema kuwa Bi. Macron alipata madai hayo kuwa "ya kuhuzunisha sana" na kwamba ni "usumbufu" kwa rais wa Ufaransa.

Bi. Owens, ambaye ni mchambuzi wa zamani wa shirika la kihafidhina la Marekani Daily Wire na ana mamilioni ya wafuasi kwenye mitandao ya kijamii, ameendelea kueneza mtazamo wake kwamba Brigitte Macron ni mwanaume.

Chapisha Maoni

0 Maoni