Dk. Nchimbi mwendo mdundo akiendelea kusaka kura za CCM mikoa ya Kanda ya Ziwa

 

MGOMBEA mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi amewasili katika uwanja wa Kashai,Bukoba mjini  kuwahutubia wananchi kwenye mkutano wa kampeni leo Septemba 7, 2025 mkoani Kagera.

Awali leo Dk. Nchimbi ameanza ziara yake ya kampeni Mkoani humo akianzia Jimbo la Ngara, Kyerwa, Katoro-Bukoba Vijijini na kuhitimisha kwa mkutano mkubwa jioni hii hapa Bukoba Mjini.

Dk. Nchimbi anaendele na mikutano  yake ya kampeni ya kusaka kula za ushindi wa kishindo kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nchi nzima,ambapo kwa sasa yuko mikoa ya Kanda ya Ziwa ambapo alianzia mkoani Mwanza, Mara, Simiyu, Shinyanga, Geita na sasa yupo mkoani Kagera.

Dk. Nchimbi anaendelea kuinadi Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu 2025-2030, ambayo inalenga kuboresha maisha ya wananchi na ustawi wa maendeleo katika miaka mitano ijayo huku akitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kumchagua mgombea Urais wa CCM, Dkt Samia Suluhu Hassan, Wabunge na Madiwani wa Chama hicho kwa kura za kishindo ifikapo Oktoba 29,2025.




Chapisha Maoni

0 Maoni