Waziri Mkuu alipongeza Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE)

 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amelipongeza Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) kwa kuongezeka kwa thamani ya soko hilo na kufikia shilingi trilioni 21.0 katika kipindi cha kufikia julai 2025.

Amesema kuwa pia soko hilo limeongeza ukuaji wa mauzo ya hisa kwa zaidi ya asilimia 246 pamoja na ongezeko la idadi ya wawekezaji hadi zaidi ya akaunti 683,000 ikiwa ni ishara ya ukuaji imara wa sekta ya mitaji nchini

Amesema hayo leo Jumanne (Agosti 26, 2025) alipotembelea Ofisi za soko hilo zilizopo Morocco, jijini Dar es Salaam.



Chapisha Maoni

0 Maoni