Katibu Mkuu wa WPL akutana na Papa Leo XIV Italia

 

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake Duniani (WPL)  na aliyekuwa Mbunge wa  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Neema Lugangira, Agosti 23,2025 amekutana, kuzungumza na kusalimiana na kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo XIV,  kwenye Makazi yake Jijini Vatican nchini Italia.

Lugangira amekutana na Papa Leo XIV siku chache baada ya kuteuliwa rasmi kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya WPL yenye makao yake makuu Jijini Brussels nchini Ubelgiji akiwa Mtanzania wa kwanza kuhudumu kwenye Jumuiya hiyo ya Kimataifa.

Lugangira ni miongoni mwa viongozi kutoka Tanzania wanaoongoza taasisi kubwa za kimataifa duniani, pamoja na mambo mengine kiongozi huyo anatajwa kuwa na uwezo mkubwa wa kiuongozi.

Chapisha Maoni

0 Maoni