‎Kanda ya Kaskazini yapewa Bilioni 139 Sekta ya Umwagiliaji mwaka wa fedha 2024/25‎

 

‎Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Queen Sendiga  amesema Serikali  imetoa jumla ya shilingi Bilioni 139 katika sekta ya Umwagiliaji katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini mwaka wa fedha 2024/25.‎

Mhe. Sendiga ameyasema hayo wakati akifungua Maonesho ya 31 ya NaneNane Kanda ya Kaskazini, Agosti 05, 2025 katika Viwanja vya Themi Njiro, Arusha ambapo alikuwa mgeni rasmi.‎

"‎Sekta ya Umwagiliaji katika Mkoa wa Arusha unatekeleza miradi ya miundombinu ya Umwagiliaji yenye thamani ya Bilioni 85.24, Mkoa wa Kilimanjaro miradi yenye thamani ya bil.39.1 na Mkoa wa Manyara miradi yenye thamani ya Shilingi bil.15.2," alisisitiza Mhe. Sendiga.‎

‎Aidha, Mhe. Sendiga amewataka wakulima  kubadilika kwa kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo ili kuweza kujipatia kipato kizuri wanapofanya shughuli  za kilimo.‎

‎Kwa upande mwingine amewaomba wadau na Taasisi mbalimbali wawafikie wakulima, wavuvi na wafugaji ili watatue changamoto zao ili waongeze tija katika sekta hizo.‎

‎Mbali na hayo, Mhe. Sendiga  amewakumbusha wananchi wote  kuchagua viongozi ambao watasimama bega kwa bega na wakulima .

Sanjari na hilo, amewaomba washiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu kwa amani, utulivu na bila kuruhusu mazingira ya kuwagawa watanzania kiitikadi, kidini au kikabila.

Kauli mbiu ya maonesho ya NaneNane 2025, " Chagua viongozi Bora kwa Maendeleo endelevu ya kilimo, mifugo na uvuvi."


              Na. Ruth Kyelula - Manyara RS

Chapisha Maoni

0 Maoni