‘Jaji mwenye huruma’ Frank Caprio afariki dunia

 

Jaji maarufu wa Marekani na nyota wa mitandao ya kijamii, Frank Caprio, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 88, familia yake imethibitisha.

Katika taaluma yake ya zaidi ya miaka 40 huko Rhode Island, alijulikana sana kwa kutumia huruma na ucheshi kutoa maamuzi yaliyotilia maanani hali binafsi za watu waliokuwa mahakamani.

Video za Jaji Caprio akihukumu kesi katika kipindi chake maarufu cha televisheni Caught in Providence zimeangaliwa na watu mabilioni kwenye mitandao ya kijamii, na kumpatia umaarufu kama "hakimu mwema zaidi duniani".

Kifo chake, kilichotokea baada ya kugunduliwa kuwa na saratani ya kongosho, kilitangazwa kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, ambako atakumbukwa kwa "upole wake" na "imani yake isiyoyumba juu ya wema wa watu".

Jaji Caprio alihudumu katika maelfu ya kesi katika mji wake wa Providence, Rhode Island, kabla ya kuanza taaluma ya runinga.

Mtindo wake wa kipekee wa uendeshaji wa kesi ulisababisha vipande vya video kusambaa kwa kasi, ikiwa ni pamoja na kumwalika mtoto wa mtuhumiwa kukaa naye nyuma ya meza ya Jaji wakati wa kesi, kusema Jaji mdogo atanisaidia kutoa hukumu.

Chapisha Maoni

0 Maoni