Harambee ya CCM yakusanya Shilingi Bilioni 86

 

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekusanya zaidi ya Sh86 bilioni katika harambee ya kukichangisha fedha kwa ajili kampeni za Uchaguzi Mkuu wa utakaofanyika Oktoba 2025 pamoja na ujenzi wa chama hicho.

Harambee hiyo imefanyika jana usiku Agosti 12, 2025 katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Mwenyekiti wa CCM, ambaye pia Rais Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akitoa ufafanuzi wa fedha hizo zilizochangishwa katika harambee hiyo Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema kati ya kiasi hicho Sh 56.3 bilioni ni fedha taslimu na Sh 30 bilioni ni ahadi. Malengo ya harambee hiyo ilikuwa ni kukusanya Sh100 bilioni.

Akiongea katika harambee hiyo Rais Dkt. Samia amewapongeza wote waliotoa fedha na kusema zitasaidia katika kampeni za uchaguzi zitakazoanzia Agosti 28 hadi Oktoba 28, 2025, ambapo siku Jumatano ya Oktoba 29, 2025 wananchi watapiga kura.


Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongea jambo na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi, wakatika wa Harambee ya CCM iliyofanyika jana usiku Agosti 12, 2025 katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.





Chapisha Maoni

0 Maoni