Kamati Kuu ya Halmashauri
ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, imepitisha jina la Naibu Waziri Mkuu na
Waziri wa Nishati Dkt. Doto Mashaka Biteko kuwa mgombea pekee wa ubunge wa Jimbo
la Bukombe kwa tiketi ya chama hicho.
Dkt. Biteko ni miongoni
wa wagombea wachache waliobahatika kupita bila ya kupata mpinzani ndani ya CCM,
ambapo wengine waliopata bahati hiyo ni pamoja na Mama Salma Rashid Kikwete Jimbo
la Mchinga, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye
Ulemavu), Ridhiwani Jakaya Kikwete Jimbo la Chalinze na Hamad Chande Jimbo la
Kojani.
Katibu wa Halmashauri Kuu
ya CCM, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, ametangaza leo Julai 29, 2025
majina yote ya wagombea waliopitishwa baada ya kuomba kupendekezwa katika
mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM.
0 Maoni