Serikali yaanza mashauriano Marekani isizuie Watanzania

 

Serikali ya Tanzania imeanza mashauriano na maafisa wa Marekani kujua maeneo yanayotakiwa kufanyiwa maboresho ili kuhakikisha Tanzania isiwe moja ya nchi ambazo raia wake watazuiliwa kuingia Marekani.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa imesema mashauriano hayo yanalenga kujua maeneo ambayo yanatakiwa kufanyiwa maboresho hususan yanayohusiana na masuala ya kikonseli.

Mashauriano haya yanakuja wakati ambapo Marekani imekuwa ikichunguza na kuweka vikwazo vya visa kwa baadhi ya nchi kutokana na masuala ya usalama na utawala bora.



Chapisha Maoni

0 Maoni