Nyota wa soka mstaafu Zlatan Ibrahimović atembelea Serengeti

 

Nyota wa Kimataifa (mstaafu) wa mchezo wa soka Zlatan Ibrahimović, aliestaafu soka katika klabu ya AC Milan ya Italia ametembelea Hifadhi ya Taifa Serengeti jana tarehe 11 Juni 2025.

Kutokana picha aliyoichapisha kwenye ukurasa wake rasmi wa Instagram (@iamzlatanibrahimovic), Ibrahimović ameonekana amekaa kwenye msingi wa jiwe hilo mkono wa kushoto kuna maandishi yaliyocharazwa “Serengeti Shall Never Die”, akifurahia mandhari ya kuvutia ya hifadhi hiyo maarufu duniani.

Ujio wa Ibrahimović nchini Tanzania ni ishara ya mvuto mkubwa wa Hifadhi za Taifa Tanzania Duniani, hususan Hifadhi ya Taifa Serengeti kwa wageni mashuhuri, na umaarifu huo unatoa fursa  ya kuitangaza sekta ya utalii ndani na nje ya Tanzania kupitia ushawishi wa watu maarufu duniani (Influencers).

Chapisha Maoni

0 Maoni