Kimwanga, achukua na kurudisha fomu kutetea udiwani Makurumla

 

Aliyekuwa Diwani wa Kata wa Makurumla Bakari Kimwanga, amechukua na kurudisha fomu kutetea udiwani Makurumla kwa kipindi kingine cha miaka mitano iwapo atapatiwa ridhaa tena na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kimwanga ambaye ameiongoza Kata hiyo ya Makurumla kwa mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitano iliyomalizika amekabidhi fomu yake hiyo leo Juni 29, 2025 kwa Katibu wa Kata wa CCM Makurumla, Omari Suleiman Bakari.

Akizungumza baada ya kukabidhi fomu hiyo, Kimwanga ambaye pia ni mwanahabari alisema kuwa anajivunia kazi kubwa aliyoifanya kwa miaka mitano na sasa anaomba fursa kwenye kukamilisha maeneo yaliyobaki ili kujenga jamii yenye ustawi.

"Ninamaliza miaka mitano ya mafanikio ambapo sisi Makurumla tumefanikiwa kutekeleza miradi ya zaidi ya shilingi bilioni 18 ikiwamo ya barabara, kituo cha afya na elimu,” alisema Kimwanga na kuongeza,

"Miaka mitano ijayo tunakwenda kujenga kata yenye kasi zaidi na muonekano mkubwa wa maendeleo kwa jamii, wana Makurumla na wana CCM ni watu wema sana nyakati zote tumekuwa pamoja na Mungu akipenda ikiwa chama itawapendeza jina likarudi kwenye uteuzi sina shaka na maamuzi yao kwangu na chama chetu ni ushindi."



Chapisha Maoni

0 Maoni