Serikali yaipatia Simba ndege ya kwenda Morocco

 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi ameliambia bunge leo Mei 08, 2025 kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itawapa timu ya Simba SC ndege kuelekea Morocco kwenye mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.

“Baada ya mafanikio makubwa ya Simba na sasa inaingia kwenye mchezo wa kwanza wa fainali ya Kombe la Shirikisho linaloandaliwa na CAF, Simba inakwenda Morocco kupambana na RS Berkane na Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Rais Dr Samia imefanya maamuzi ya kutoa ndege itakayoipeleka Klabu ya Simba Morocco kwa ajili ya mchezo huo,” amesema Prof. Kabudi.

Amesema kwamba Serikali imefanya uamuzi huo ikiwa ni sehemu za jitihada za Serikali za kuipunguzia Simba umbali wa safari na uchovu, Simba SC kwenda Morocco kwa ndege ya abiria kungewafanya wazunguuke na kutumia muda mwingi njiani kutokana na kulazimika kupita nchi tofautitofauti kwa ajili ya kuunganisha ndege.

Hii sio mara ya kwanza kwa Rais Samia kuzisaidia timu za Tanzania Kimataifa (Simba na Yanga) ili kuhakikisha zinafanya vizuri na kuitangaza nchi. Mwaka jana Yanga ilipofuzu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, Rais Samia alitoa ndege iliyoipeleka timu hiyo Algeria na kuirudisha Dar es Salaam.

Chapisha Maoni

0 Maoni