Rais Donald Trump amuita Putin mwendawazimu

 

Rais wa Marekani, Donald Trump, amemuita Vladimir Putin "mwendawazimu kabisa" kufuatia mashambulizi makubwa ya anga ya Urusi dhidi ya Ukraine yaliyofanywa mwishoni mwa wiki.

"Anaua watu wengi bila sababu, na sizungumzii tu wanajeshi. Makombora na droni yanapigwa kwenye miji ya Ukraine bila sababu yoyote," Trump aliandika kwenye mtandoa wake wa jamii siku ya Jumapili.

Ingawa hasira zake zilielekezwa hasa kwa rais wa Urusi, Trump pia alikuwa na maneno makali kwa Zelensky, akisema kuwa "hafanyi lolote la msaada kwa nchi yake kwa kuzungumza jinsi anavyofanya."

Usiku wa Jumamosi, Urusi ilirusha droni na makombora 367 dhidi ya Ukraine, shambulizi kubwa zaidi la anga dhidi ya Ukraine tangu kuanza kwa uvamizi kamili mwaka 2022. Watu wasiopungua 12 waliuawa.

Chapisha Maoni

0 Maoni