Moshi mweupe huoo, ni Mmarekani Papa Leo XIV

 

Papa mpya Robert Prevost, ambaye atajulikana kama Papa Leo XIV, amekuwa Mmarekani wa kwanza kuchaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki duniani.

Prevost, 69, ambaye baba yake anaasili ya Ufaransa na mama yake Italia, amejitokeza baada ya kuchaguliwa na kuwasalimia maelfu ya watu waliokusanyika St Peter's Square.

“Amani iwe kwenu wote,” alisema Papa Leo XIV akiwasalimu watu akiwa kwenye kibaraza cha Vatican.

Prevost mzaliwa wa Chicago Marekani ni mwanamabadiliko na amefanya kazi kwa miaka mingi kama mmishenari huko Peru kabla ya kuwa Askofu akiwa huko.

Chapisha Maoni

0 Maoni