Serikali ya CCM kuboresha hali ya vyombo vya habari nchini

 

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema atahakikisha katika Ilani ya uchaguzi ya CCM inakuwa na eneo la kuboresha hali ya vyombo vya habari nchini.

Dkt. Nchimbi ameyasema hayo leo mkoani Songea wakati akifungua Mkutano Mkuu Maaluma wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), ambapo amesema vyombo vya habari ni muhimu kwa mustakabali wa taifa.

“Tumeshaanza kuandaa Ilani ya uchaguzi ya CCM na kunamaboresho tunafanya, hivyo basi nawaahidi kuwa nitahakikisha Ilani ya uchaguzi inakuwa na eneo la kuboresha hali ya vyombo vya habari nchini,” amesema Dkt. Nchimbi.

Pamoja na mambo mengine mesema Serikali ya CCM inatambua mchango wa vyombo vya habari nchini na kuvipongeza vyombo hivyo kwa kuwa makini katika kuhabarisha jamii jambo ambalo limechangiwa kuwepo kwa amani nchini.

“Amani katika nchi hii inajengwa na jinsi mnavyoandika habari katika vyombo vyenu vya habari...leo tunaamani na mshikamano kwa sababu ya kazi kubwa mliyoifanya,” amesema Dkt. Nchimbi.

Aidha, Dkt. Nchimbi amewaasa waandishi wa habari nchini kuhakikisha kuwa wakati wa kuelekea katika uchaguzi mkuu wa 2025 hawatoi habari ambazo zinaweza kuhatarisha amani ya nchi.

“Mkimkuta mtu anaongelea masula ya kuhatarisha amani ya nchi ama kuchochea uvunjifu wa amani, msiandike habari zake, mziache mpite tu kama mmemkuta kichaa akisema maneno ya hovyo mtaani,” amesema Dkt. Nchimbi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TEF Deodatus Balile pamoja na kuipongeza serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha uhuru wa vyombo vya habari nchini, ameiomba serikali kutatua changamoto ya hali mbaya ya uchumi wa vyombo vya habari nchini.

“Tunaomba serikali iwe na sera maalum ya kuendeleza vyombo vya habari nchini, jambo hili sio geni hata katika mataifa mengine linafanyika hilo,” amesema Balile.

Chapisha Maoni

0 Maoni