Rais Samia awatunuku nishani viongozi mbalimbali

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimtunuku Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Pili kwa Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohamed Ali Shein, kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 26 Aprili, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimtunuku Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Pili kwa Makamu wa Pili wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Ali Idd kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 26 Aprili, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mwakilishi wa Familia ya Hayati Edward Ngoyai Lowassa Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Pili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 26 Aprili, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimtunuku Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Pili kwa Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Awamu ya Nne Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 26 Aprili, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimtunuku Nishani ya Kumbukumbu ya Muungano Daraja la Pili kwa Spika Mstaafu wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe. Pandu Ameir Kificho kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 26 Aprili, 2025.


Chapisha Maoni

0 Maoni