JK awasilisha ujumbe wa Rais Samia kwa Rais Museveni

 

Rais Mstaafu wa Tanzania Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha ujumbe maalum kwa Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kutoka kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Kikwete amewasilisha ujumbe huo maalum, pembenzoni mwa Mkutano wa Uongozi wa Afrika wa nane unaofanyika jijini Kampala nchini Uganda.

Kwa upande wake Rais Museveni alimshukuru kwa ziara na kumuomba amfikishie salamu zake kwa Mheshimiwa Rais Samia na watu wa Tanzania.



Chapisha Maoni

0 Maoni