Hashim Lundenga afariki dunia

 

Aliyekuwa mwaandaji wa mashindano ya Miss Tanzania Hashim Lundenga amefariki dunia asubuhi ya leo 19/04/1015 katika hospitali ya Kitengule iliyupo Tegeta Jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa mshirika wa karibu wa Marehemu Lundenga, Bosco Majaliwa, Lundenga ambaye amekuwa akiumwa kwa muda mrefu, alikimbizwa hospitalini hapo leo asubuhi baada ya kuzidiwa lakini muda mfupi baadaye akafariki.

“Hapa ndiyo tunafanya utaratibu wa kuuchukua mwili kwenda kuuhifadhi halafu turudi nyumbani Boko kupanga taratibu za mazishi,” alisema Bosco kwa masikitiko.

Chapisha Maoni

0 Maoni