Aliyesababisha kifo cha SP Chiko Dar akamatwa Mbeya

 

Jeshi la Polisi limemkamata Elia Asule Mbugi (25) marufu kama Dogo bata mkazi wa Segerea dereva aliyekuwa akiendesha gari namba T 580 EAE aina TATA Daladala lililosababisha kifo cha SP Awadh Ramadhani Chico aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya kipolisi Chanika.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa na makachero wa Polisi  Kanda maalum ya Dar es Salaam tarehe 27 Machi 2025 maeneo ya Mbalizi Mkoani Mbeya, na atafikishwa  mahakamani haraka iwezekanavyo. 

Dereva huyo alikuwa akisakwa na Polisi Jijini Dar es Salaam tangu tarehe 17  Machi 2025 ilipotokea ajali hiyo iliyosababisha kifo cha SP Chico, kufuatia  kutoroka mara tu baada ya kugonga gari na kusababisha kifo.

Chapisha Maoni

0 Maoni