TAWIRI yajikita Korogwe na Mkinga kutatua migongano ya binadamu na mamba

 

Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii wamepiga kambi Mkoani Tanga, Wilaya ya Korogwe kijiji cha Kwaisewa na Wilayani Mkinga kijiji cha Kwangena vinavyokabiliwa na changamoto ya Mamba.

Timu hii ya wataalamu wanaendelea kutathmini athari na madhara yaliyojitokeza kutokana na uwepo wa Mamba katika maeneo ya moto wananchi wanapopata huduma ya maji.  Tathmini imefanyika kwa kushirikiana na wananchi na ujenzi wa vizimba unaendelea katika maeneo husika.

TAWIRI imefanya tathmini ya maeneo husika kupitia vikao na viingozi wa Wilaya na vijiji husika ili kuondoa adha hii, kizimba Kimoja kitajengwa kijiji cha Kwaisewa - Korogwe Katika Mto Pangani - Ruvu eneo la Lang'ata na Kizimba kimoja kijiji cha Kwangena Wikayani Mkinga, pembezoni mwa mto Zigi.

Maeneo haya ni maeneo muhimu sana ambapo wanajamii hupata huduma ya maji kila siku kwa matumizi ya binadamu na mifugo lakini pia ni maeneo hatarishi kwa mamba. Wananchi hawa kwa sasa hawana   huduma ya maji ya Bomba wala visima hivyo hutegemea makji ya mto.

Akishukuru kwa niaba ya viongozi, Mhe. Aloyce Kundema, Diwani wa Kata ya Mnyenzini Wilaya ya Mkinga, alisema hakika msaada huu umekuja muda muafaka kwani wananchi wengi hasa watoto wamepoteza maisha na wengine kupata vilema vya kudumu kufuatia adha ya Mamba. Aidha amepongeza juhudi za Wizara ya Maliasili nanutalii kuleta.msaada huu, anaamini hii itakuwa suluhu hasa katika kuokoa maisha ya wananchi.

Kazi hii inategemewa kukakimilika ndani ya wiki mbili, vizimba vitakabidhiwa rasmi kwa viongozi husika ngazi ya Wilaya, na elimu zaidi ya matumizi ya vizimba, na namna ya kujiokoa dhidi ya uvamizi wa Mamba itaendelea kutolewa.



Chapisha Maoni

0 Maoni