Msajili wa Hazina azindua huduma ya uwekezaji wa hisa kidijitali

 

Msajili wa Hazina Bw. Nehemiah Mchechu amezindua huduma mpya ya uwekezaji wa hisa kupitia Popote Mobile App.

Huduma hii itawawezesha wateja kununua, kuuza na kuangalia mwenendo wa bei za hisa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Huduma hiyo mpya ambayo ni zao la ushirikiano kati ya benki ya TCB na DSE, ilizinduliwa jana Ijumaa, Februari 21, 2025, jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi wa huduma hii unakuja katika wakati ambapo soko la mitaji la Tanzania linahitaji mageuzi ya kidijitali ili kuongeza ushiriki wa wananchi.

Popote Mobile App ni suluhisho la kisasa ambalo linaruhusu Watanzania kufanya miamala ya hisa kupitia simu zao za mkononi, hali itakayochochea ukuaji wa uchumi na kupanua fursa za uwekezaji katika masoko ya mitaji.

Chapisha Maoni

0 Maoni