JKCI kufanya matibabu ya mishipa ya damu kutanuka kwenye miguu

 

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imepanga kutoa matibabu kwa wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya damu kutanuka kwenye miguu kwa jina la kitaalamu ‘Varicose Vein’ katika kambi maalumu ya uchunguzi na matibabu ya kutanuka kwa mishipa hiyo.

Taarifa iliyotolewa na JKCI imesema kwamba matibabu hayo yatakayotolewa kuanzia tarehe 12 hadi 15 Februari 2025 na yatafanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Andalusia ya nchini Misri.

JKCI imewaomba wataalamu wa afya nchini kutoka Hospitali za Wilaya, Mikoa na Rufaa kuwatuma wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya damu kutanuka kwenye waje kutibiwa katika kambi hiyo maalumu na kupatiwa tiba.

Matibabu yatakayofanyika katika kambi hiyo ni ya upasuaji kwa njia ya kutumia matundu madogo katika kutibu mishipa ya damu ya vein iliyotanuka kwa kutumia kifaa cha umeme kijulikanacho kwa jina la laser ablation machine, imeeleza taarifa hiyo ya JKCI.

Chapisha Maoni

0 Maoni