Wadau wahimizwa kutumia mfumo wa NeST katika manunuzi

 

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Mhandisi Chagu Ng'homa amewataka wadau wa ununuzi nchini kuutumia ipasavyo mfumo mpya wa Kielektroniki wa Manunuzi ya Umma (NeST), ili kusaidia kupata wazabuni zenye gharama zinazolingana na thamani ya fedha zinazolipwa.

Ng’homa ametoa wito huo leo tarehe 20 januari, 2025 kwa niaba ya  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza wakati akifungua mafunzo yaliyofanyika Rock City Mall- Mwanza ya mfumo wa Usimamizi na Ununuzi wa Umma Kielektroniki yaliyowakufanisha washiriki kutoka taasisi mbalimbali nchini.

Amesema, washiriki wanapaswa kuwa wazalendo kwenye kazi zao kwa kuzingatia kuwa wanatakiwa kulinda rasilimali fedha za nchi wakati wa ununuzi kwa kuwashindanisha wazabuni kwa mujibu wa sheria.

"Mfumo huu umeletwa mahsusi ili kusaidia kuongeza wigo wa ushiriki wa wazabuni, kukidhi mahitaji na matarajio ya watumiaji pamoja na kurahisisha mchakato wauombaji zabuni hivyo nendeni mkazingatie hayo ili kulisaidia taifa," amesema Chagu.

Aidha, ametoa wito kwa Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA) kuendelea kuboresha mfumo wa NeST ili  kuweka mazingira rafiki kwa wazabuni na kutoa mafunzo kwa taasisi za ununuzi ili kufikia malengo yalivyokusudiwa.

Vilevile, ametoa pongezi kwa mamlaka hiyo kwa jinsi wanavyoendelea kuboresha mfumo huo ambao Mhe. Rais Samia mwenyewe aliuzindua mahususi kwa ajili ya wadau kufuatilia mchakato kwa uwazo na kuona thamani ya fedha.

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa PPRA Robert Kalunde amesema wameandaa mafunzo hayo ya siku 5 yanayowakutanisha washiriki zaidi ya 230 kutoka taasisi mbalimbali nchini ili waujue vizuri mfumo huo na kufikia malengo kwenye ununuzi.





Chapisha Maoni

0 Maoni