Trafiki waliorekodiwa wakichukua rushwa wakamatwa

 

Jeshi la Polisi nchini limewakamata askari wawili wa kikosi cha usalama bararani waliorekodiwa wakichukua rushwa hadharani kutoka wa madereva wa daladala na kusema kuwa watachukuliwa hatua za kali za kinidhamu za mashtaka ya kijeshi.

Akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amesema kwamba askari hao mmoja mwanaume na mwingine mwanamke tayari wamekamatwa na wapo mahabusu.



Chapisha Maoni

0 Maoni