NMT yaona fursa Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa nchi za Afrika

 

Taasisi ya Makumbusho ya Taifa la Tanzania (NMT) imesema kuwa imejiandaa kutumia fursa ya ugeni wa Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika kunadi vivutio pamoja na historia ya Taifa la Tanzania kwa wageni hao.

Kauli hiyo imetolea leo na MNT, kwenye mahojiano yaliyofanyika kwenye kituo cha televisheni cha Star TV yaliyowashirikisha Mhifadhi historia Bw. Shomari Rajabu na Afisa Utalii Bi. Antonia Mnkama.

Kupitia mkutano huo utakaofanyika tarehe 27 na 28 Januari jijini Dar es Salaam, Makumbusho ya Taifa la Tanzania imejipanga kuwatembeza wageni wa mkutano huo katika maeneo ya kihistoria yanayopatikana jijini Dar es Salaam ikiwemo vituo vyake vya Kijiji cha Makumbusho na Nyumba ya utamaduni.

Chapisha Maoni

0 Maoni